ads
Mji muhimu wa mwisho uliokuwa mikononi mwa kundi la Al Shabaab kusini magharibi mwa Somalia wa Baardheere umechukuliwa tena na vikosi vya Muungano wa Afrika (AU) -miaka 7 baada ya wapiganaji hao wenye itikadi kali kuingia kwa mara ya kwanza katika mji huo .
Wakazi wa mji huo wamesema vikosi vya Kenya na Somalia vikiwa na silaha nzito na usaidizi wa mashambulizi ya anga viliuvamia mji huo , ambao wapiganaji wa Al Shabaab waliutoroka usiku.
Vikosi vya AU nchini Somalia, na vile vya jeshi la Somalia, vilifanikiwa kuuteka mji huo baada ya mashambulizi makali. Majeshi kutoka Kenya, Somalia na Ethiopia yamekua yakiendesha harakati za kuuteka mji wa Baadheere kwa siku chache zilizopita.


Kumekuwa na mapigano makali viungani mwa mji huo, lakini wanamgambo wa Alshaabab walisalim amri na kuukimbia ,na hivyo kutoa fursa ya mji huo kuchukuliwa bila mapigano .
Wakazi wanasema kamanda mmoja wa Somali na vyombo vya habari vinavyounga mkono Al Shabaab wamethibitisha kuchukuliwa kwa mji huo.


Harakati hizo za kuuteka mji wa Baadheere zimefanikiwa siku chache kabla rais wa Marekani Barack Obama kufanya ziara Afrika mashariki ambapo suala la usalama nchini Somalia litakuwa kwenye ajenda kuu za ziara yake .
Kundi la Al shaabab lina uhusiano na mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda linapigana dhidi ya serikali ya Somalia kwa ajili ya udhibiti wa nchi hiyo.
Wiki iliyopita mashambulizi ya ndege zisizokua na rubani (drone) zilizoshambulia ziliripotiwa kuwauwa makamanda wa ngazi ya juu wa Al Shabaab.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: